"UTAFITI UNAONYESHA KWAMBA MITANDAO YA KIJAMII INACHANGIA UPWEKE"
Nadharia za ripoti hiyo zinaelezea kwamba kwa jinsi unavyotumia muda mwingi kwenye mtandao wa kijamii, ndivyo unavyotumia muda mdogo kufikiria mawasiliani halisi ya dunia.
Matumizi ya mitandao ya mawasiliano ya kijamii pia yanaweza kusababisha hisia za kutengwa, kama vile kuona picha za marafiki zako wakifurahia tukio fulani ambalo wewe hukualikwa.
Wataalam hao wa Saikolojia waliwahoji watu wazima takriban 2,000 walio na umri wa miaka kati ya 19 - 32 kuhusu matumizi yao ya mitandao ya mawasiliano ya kijamii.
Profesa Brian Primack, kutoka Chuo Kikuu cha tiba cha Pittsburgh, alisema: " Hili ni suala muhimu kulichunguza kwasababu matatizo ya afya ya akili na kutengwa na jamii yamefikia katika viwango vya mlipuko miongoni mwa vijana.
" Sisi ni viumbe tulioumbwa kuishi kijamii, lakini maisha ya kisasa yanatufanya tutengane baada ya kutuleta pamoja.
"huku ikionekana kuwa mitandao ya kijamii inatoa fursa ya watu kuishi kama jamii, nadhani uchunguzi huu unaonyesha kuwa huwenda isiwe suluhu ambalo watu walilitegemea."
Nadharia za ripoti hiyo zinaelezea kwamba kwa jinsi unavyotumia muda mwingi kwenye mtandao wa kijamii, ndivyo unavyotumia muda mdogo kufikiria mawasiliani halisi ya dunia.
Matumizi ya mitandao ya mawasiliano ya kijamii pia yanaweza kusababisha hisia za kutengwa, kama vile kuona picha za marafiki zako wakifurahia tukio fulani ambalo wewe hukualikwa.
Wataalam hao wa Saikolojia waliwahoji watu wazima takriban 2,000 walio na umri wa miaka kati ya 19 - 32 kuhusu matumizi yao ya mitandao ya mawasiliano ya kijamii.
Profesa Brian Primack, kutoka Chuo Kikuu cha tiba cha Pittsburgh, alisema: " Hili ni suala muhimu kulichunguza kwasababu matatizo ya afya ya akili na kutengwa na jamii yamefikia katika viwango vya mlipuko miongoni mwa vijana.
" Sisi ni viumbe tulioumbwa kuishi kijamii, lakini maisha ya kisasa yanatufanya tutengane baada ya kutuleta pamoja.
"huku ikionekana kuwa mitandao ya kijamii inatoa fursa ya watu kuishi kama jamii, nadhani uchunguzi huu unaonyesha kuwa huwenda isiwe suluhu ambalo watu walilitegemea."
0 comments:
Post a Comment